Jalada la maelezo fafanuzi: Lishe ya Mtoto nchini Tanzania
Hali ya lishe ya watoto
· Tatizo la utapiamlo hususani udumavu (kuwa na kimo kidogo ukilinganisha na umri) miongoni mwa
watoto wenye umri wa chini ya miaka 5, limepungua toka asilimia 50 mwaka 1992 hadi
kufikia asilimia 35 mwaka 2014, ambapo imeathiri watoto takriban milioni 2.7. Kulingana na vigezo
viliyoainishwa na Shirika la Afya Duniani (mwaka 1995), tatizo la udumavu limepungua toka “hali
ya juu kabisa” kufikia “hali ya juu”.
· Hatua madhubuti kabisa za kuwakinga watoto
dhidi ya udumavu zinafanyika katika kipindi cha dhana iliyoitwa ‘ dirisha la
fursa ’ yaani kuanzia kutungwa kwa mimba, kipindi cha ukuaji wa mimba hadi
mwisho wa kipindi cha miaka miwili ya uhai wa mtoto.
· Tatizo la utapiamlo mkali wa jumla au hali ya ukondefu kwa watoto ( kuwa na
uzito mdogo ukilinganishwa na kimo cha mtoto) chini ya umri wa miaka 5 ilipungua
toka asilimia 8 ngazi ya kitaifa mwaka 1992 hadi kufikia asilimia 4 mwaka 2014.
Tatizo la utapiamlo mkali liko katika kiwango cha “chini kabisa” kulingana na vigezo
vya Shirika la Afya Duniani. Hata
hivyo, visiwani Zanzibar, kiwango cha utapiamlo mkali wa jumla kilbaki kuwa juu, na kinafikia
asilimia 7.
· Kulingana na idadi halisi, zaidi ya watoto
430,000 wenye umri wa chini ya miaka mitano
wanasumbuliwa na utapiamlo mkali wa jumla, miongoni mwao zaidi ya watoto 100,000 wana utapiamlo mkali sana, na kati ya
asilimia 5-20 ya watoto hao wako katika hali hatarishi inayoongeza uwezekano wa
kufa .
· Tatizo la upungufu wa uzito usiokuwa wa kawaida kwa
watoto chini ya umri wa miaka mitano limepungua toka asilimia 25 mwaka 1992 hadi
kufikia asilimia 13 mwaka 2014, idadi ambayo inakaribia asilimia 12.5 ikiwa lengo ambalo serikali ya
Tanzania imejiwekea.
· Utapiamlo umetawanyika kwa viwango tofauti
baina ya mikoa na jinsia tofauti nchini Tanzania, hasa ukiwaathiri zaidi
wavulana, watoto wanaoishi katika jamii zenye mapato duni na miongoni mwa watoto
wanaoishi katika mikoa mahsusi[1].
· Mifano miwili ya taratibu muhimu za malezi ya watoto kwa
ajili ya lishe bora katika maisha ya mtoto mchanga ni Unyonyeshaji na ulishaji wa chakula
cha nyongeza , ila tabia na taratibu
za ulishaji wa watoto wachanga na watoto wenye umri mdogo bado ni hafifu:
o Kiwango cha unyonyeshaji mtoto maziwa ya mama pekee katika
miezi 6 ya mwanzo (EBF) miongoni mwa
watoto wenye umri kati ya miezi 0-5 kiliongezeka toka asilimia 29 mwaka 1996 hadi
kufikia asilimia 41 mwaka 2005, ila idadi ya asilimia hii haikubadilika na
kubaki asilimia 42 mwaka 2014. Visiwani Zanzibar, ni asilimia 20 tu ya watoto
wenye umri wa chini ya miezi 6 wananyonyeshwa bila kuchanganya maziwa ya mama na
vitu vingine. Asilimia 51 ya watoto Tanzania Bara na asilimia 62 Visiwani Zanzibar wananyonyeshwa katika kipindi cha
saa ya kwanza baada ya kuzaliwa;
o
Kuhusu
ulishaji watoto vyakula vya nyongeza,
asilimia 25 ya watoto wenye umri wa kati ya miezi 6-23 wanapata chakula cha mchanganyiko wa
vyakula mbalimbali kwa Tanzania Bara dhidi ya asilimia 12 Visiwani Zanzibar. Hali
kadhalika, ni asilimia 20 tu ya watoto Tanzania Bara
wanapata milo yenye mchanganyiko wa vyakula mbalimbali na kulishwa idadi ya
milo inayokubalika dhidi ya asilimia 8 Visiwani Zanzibar. Idadi ya watoto kitaifa wanaopata wastani wa
milo inayopendekezwa kwa siku ni asilimia 66 kwa Tanzania bara na na asilimia 54 Visiwani Zanzibar.
·
Upungufu ya virutubishi ni tatizo la kawaida na mikakati ya
kushughulikia tatizo hilo inaonyesha maendeleo yanayo badilika mara kwa mara:
o
Tatizo
la upungufu wa damu miongoni mwa watoto wenye
umri wa chini ya miaka mitano ulipungua toka asilimia 72 mwaka 2005 hadi
kufikia asilimia 59 mwaka 2010;
o
Theluthi moja ya watoto
wanaathirika na upungufu wa vitamini (asilimia
33);
o
Ni
asilimia 8.3 tu ya wanawake walio katika umri wa kuzaa wenye watoto chini ya miaka
mitano waliwahi kutumia vidonge vya madini
ya chuma na asidi ya foliki (iron-folic acid) katika
kipindi cha siku 90 au zaidi wakati wa ujauzito wao uliopita, kama inavyoagizwa
na Shirika la Afya Duniani (WHO);
o
Vitamini A ni muhimu sana kwa ajili ya uimarishaji wa mfumo
wa kinga, na matumizi ya ziada ya Vitamini A yanaweza kupunguza vifo vya watoto
kabisa. Uwiano wa watoto wenye umri kati ya miezi 6-59 wanaopata Vitamini A ya
ziada ulipanda toka asilimia 61 mwaka 2010 na kufikia asilimia 72 mwaka 2014. Hata hivyo, matumizi yake yalipungua Zanzibar toka asilimia 79 mwaka
2010 hadi kufikia asilimia 61 mwaka 2014.
o
Uwiano
wa watoto wenye umri kati ya miezi 12-59 wanaopata vidonge vya kukabiliana na minyoo uliongezeka toka asilimia 50 mwaka 2010 hadi asimilia 71 mwaka 2014, ila ulipungua Visiwani Zanzibar toka
asilimia 72 mwaka 2010 na kufikia asilimia 68 mwaka 2014[2].
Sababu
na madhara ya lishe duni
· Watoto wanaweza kupatwa na utapiamlo ikiwa watasumbuliwa
na magonjwa yanayosababishwa na lishe duni au ikiwa hawana uwezo wa kula
chakula cha kutosha na cha mchanganyiko. Mara nyingi sababu hizi mbili zinatokea
kwa pamoja na zinatokana na sababu nyingi zilizojificha, zikijumuisha upatikanaji
usiojitosheleza au kutokupatikana kwa chakula au kutokuwepo na fursa za
kiuchumi, huduma duni za kiafya, mazingira yasiyokuwa rafiki kiafya na shughuli
za malezi zisizotosheleza kwa watoto na
wanawake.
· Watoto wenye utapiamlo wana athirika zaidi na magonjwa ya
maambukizi na viwango vya juu vya vifo miongoni mwa watoto hawa. Zaidi ya hayo,
utapiamlo unaathiri ukuaji wa ubongo na huwa unapunguza uwezo wa kiakili na wa
kujifunza miongoni mwa watoto, hali ambayo inasababisha uwezo hafifu mashuleni
na kupunguza mapato ya kiuchumi wanapokua watu wazima.
· Utapiamlo unatafsiriwa katika upotevu wa kiuchumi wa mtu
mmoja mmoja hadi kufikia asilimia 10 ya Jumla ya Pato la Taifa (GNP) na
kuathiri ukuaji wa uchumi wa nchi.
· Tatizo la
utapiamlo kwa watoto linaweza kupungua kwa kupitia mtazamo unaojumuisha sekta
nyingi, ukiunganisha hatua maalumu za kupanua huduma za lishe zinazotoa manufaa
ya moja kwa moja kwa jamii kisekta au huduma zinazohusiana na lishe
zinazofanywa na sekta mbalilmbali pamoja na kuimarisha mazingira yatakayoleta
ufanisi katika kuboresha lishe .
[1] Asilimia 58 ya watoto waliodumaa wako katika mikoa ya 10: Kagera,
Kigoma, Mbeya, Mwanza, Dodoma, Morogoro, Geita, Dar-Es-Salaam, Tabora na Ruvuma. Wengi wa watoto wanaoathirika na utapiamlo mkali
wanapatikana Dar es Salaam, Rukwa, Mwanza, Simiyu.
[2] Takwimu zote katika jalada hili la maelezo ni matokeo ya
tafiti zInazohusu Ongezeko la Watu na taarifa za Kiafya, tafiti zinazofanyika
kila baada ya miaka 5 nchini Tanzania toka Utafiti wa Kitaifa wa Lishe wa mwaka
2014
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni