Ujumbe Maalum na
Matokeo

·
Kunyonyesha maziwa ya mama kuna faida kubwa kwa wanawake na watoto kwenye
nchi zenye vipato vya chini na vya juu, na ushahidi sasa ni imara zaidi kuliko
siku za nyuma.
·
Faida za kiafya na kiuchumi za kunyonyesha maziwa ya mama ni kubwa:
kuongeza viwango vya unyonyeshaji maziwa ya mama kunaweza kuokoa maisha ya maelfu ya watu na kuongeza mabilioni ya dola kwenye uchumi wa dunia kila
mwaka.
·
Kuongeza viwango vya unyonyeshaji maziwa ya mama duniani kote ni kichochezi
cha msingi cha kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu ifikapo mwaka 2030. Kunyonyesha
maziwa ya mama kunachangia kwa kiasi kikubwa katika kuboresha lishe, elimu, na
afya ya mama mjamzito na mtoto na kuendelea kuishi kwa mama na mtoto.
·
Maendeleo kwa kasi yanawezekana, na tunajua nini kinahitaji kufanyika—nchi
nyingi zaidi zinahitaji kuwekeza kwenye sera na mipango ambayo inaunga mkono
maamuzi ya wanawake kunyonyesha maziwa ya mama.
Kunyonyesha maziwa ya mama
kuna faida nyingi sana kwa wanawake na watoto, bila kujali kama wanaishi kwenye
nchi yenye kipato cha juu au cha chini au kwenye kaya tajiri au maskini.
·
Kunyonyesha maziwa ya mama kunaokoa maisha na kuboresha afya.
o Kama njia ya kuwapa watoto lishe iliyotengenezwa
kikamilifu, maziwa ya mama ni dawa bora zaidi inayotibu kwa kuangalia mahitaji
binafsi ya lishe ya mtoto.
o Kuboresha unyonyeshaji kunaweza kuokoa takriban maisha 820,000 kwa mwaka, 87% kati yao wakiwa watoto wachanga wenye umri
wa chini ya miezi 6.
o Karibu nusu ya matukio yote ya kuhara na theluthi moja ya maambukizo yote
ya njia ya hewa yanaweza kuzuilika kwa kuongeza kiwango cha kunyonyesha maziwa
ya mama kwenye nchi zenye kipato cha chini na cha kati.
o Kuna ushahidi mkubwa zaidi kuwa kunyonyesha maziwa ya mama kunapunguza kuwepo
kwa matatizo ya unene/uzito mkubwa na
kisukari baadaye maishani.
·
Kunyonyesha maziwa ya mama kunawaandaa watoto kuwa na maisha yenye ustawi ukubwani.
o Kunyonyesha maziwa ya mama kumehusishwa na kufanya vizuri zaidi kwenye vipimo
vya upeo wa kiakili kwa watoto na vijana (wastani wa alama 3), kwa kuzingatia
mchango wa mama katika upeo wa kiakili wa mtoto.
o Baadhi ya tafiti zinaonyesha kwamba kuwa na akili kama matokeo ya
kunyonyeshwa maziwa ya mama kunapelekea kuwa na maendeleo mazuri ya kielimu,
kipato na uzalishaji mkubwa katika kipindi cha muda mrefu.
o Kidunia, makadirio ya gharama ya upeo mdogo wa kiakili unaohusika na
kutonyonyeshwa maziwa ya mama ni jumla ya takriban dola za kimarekani bilioni
300 kwa mwaka (ikiwakilisha 0.49% ya pato la jumla la nchi duniani, au GNI).
-
Nchi zenye kipato cha juu zinapoteza zaidi ya dola bilioni 230 kwa mwaka (0.53% yapato la jumla la nchi) kwa sababu ya
viwango vidogo vya unyonyeshaji maziwa ya mama.
-
Nchi zenye kipato cha chini na cha wastani zinapoteza zaidi ya dola bilioni
70 kwa mwaka (0.39% ya pato la jumla la nchi) kwa sababu ya viwango vidogo vya
kunyonyesha maziwa ya mama.
·
Kunyonyesha maziwa ya mama pia kuna faida kwa afya ya mama.
o Kwa kila mwaka ambao mama
ananyonyesha, uwezekano wa yeye kupata saratani ya matiti ya hatua ya pili
unapungua kwa 6%. Kunyonyesha maziwa ya mama pia kunapunguza hatari ya
kupata saratani ya mfuko wa mayai.
o Viwango vya sasa vya kunyonyesha maziwa ya mama tayari vinazuia vifo karibu
20,000 vinavyotokana na saratani ya matiti kila mwaka, na vifo vingine 20,000 vinaweza
kuzuiliwa kwa kuboresha namna za kunyonyesha maziwa ya mama.
Pamoja na faida za
kiuchumi, na kiafya za kunyonyesha
maziwa ya mama zinakadiriwa kuchangia kushusha gharama za mwaka za huduma ya afya
kwa jumla ya dola milioni 312 nchini
Marekani, dola milioni 48 nchini
Uingereza, dola milioni 6 nchini Brazil na
dola milioni 30.3 Uchina mjini.
Ingawa kuna ushahidi huu
mkubwa zaidi, wanawake duniani kote hawana msaada wanaohitaji kunyonyesha
maziwa ya mama.
·
Sheria zisizokidhi au kukosekana
kabisa kwa sheria zinazolinda au kutetea kipindi cha uzazi kunazuia wanawake
wengi kunyonyesha maziwa ya mama kwa kiasi kinachotakiwa.
o Likizo fupi ya uzazi
(mfano wiki6) kwa baadhi ya nchi inaongeza uwezekano wa kutonyonyesha maziwa ya
mama au kuacha kunyonyesha maziwa ya
mama mapema kwa 400%.
o Ni asilimia 23% (chini ya robo) ya nchi zote duniani zinakidhi mapendekezo ya Shirika la
Kimataifa la Kazi ya kuweka majuma 18 kwa ajili ya likizo ya uzazi.
·
Mapungufu kwenye ujuzi na uelewa wa
watoa huduma ya afya mara nyingi huwaacha wanawake bila taarifa au msaada
sahihi.
·
Mila na desturi za kifamilia na kijamii pia zina ushawishi mkubwa kwenye
maamuzi wa wanawake kunyonyesha maziwa ya mama. Yatupasa kujenga hali mpya itakayowawezesha
wanawake kuungwa mkono kuhusu maamuzi
yao ya kunyonyesha maziwa ya mama – nyumbani, kazini na kwenye jamii.
·
Uuzaji unaofanywa na tasnia kubwa na inayozidi kukua ya chakula cha mbadala
ya maziwa ya mama pia unadhoofisha kunyonyesha maziwa ya mama.
o Kati ya mwaka 2014 na
2019, mauzo ya dunia ya chakula cha mbadala ya maziwa ya mama yanatarajiwa
kuongezeka kutoka dola bilioni 45 hadi dola bilioni 71.
o Mashariki ya Kati, Afrika, na kanda ya Asia ya Pasifiki ndio maeneo ambayo
kukua kunategemea kuongezeka, ikikadiriwa kuongezeka kwa asilimia 7% na 11%.
Viwango vya kunyonyesha
maziwa ya mama havijaongezeka kwa kiasi kikubwa katika miongo miwili iliyopita,
na nchi nyingi hazielekei kufikia malengo yaliyowekwa kidunia.
·
Watoto wote walio chini ya miezi 6 wanapaswa kunyonyeshwa maziwa ya mama
bila kuchanganyiwa chakula kingine kwa miezi 6 ya mwanzo, lakini ni 37% tu
wanatimiza lengo hili kwa sasa. Lengo la dunia ni kuongeza viwango vya
kunyonyesha maziwa ya mama bila kuchanganyiwa chakula kingine kwa miezi 6 ya
kwanza ifike angalau 50%.
·
Kiwango kidogo cha kunyonyesha maziwa ya mama kulingana na mapendekezo
kunaathiri nchi zenye kipato cha juu na nchi zenye kipato cha chini pia.Unyonyeshaji
maziwa ya mama ni mojawapo ya viashiria vichache vya kiafya ambapo nchi zenye kipato
cha chini zinakaribia kufikia mapendekezo ya kimataifa kuliko nchi zenye kipato
cha juu.
o Kwa kila mara Pato la Jumla la Ndani linavyoongezeka mara mbili zaidi,
unyonyeshaji maziwa ya mama kwa miezi 12 unapungua kwa alama za asilimia
10.
o Chini ya 20% ya watoto kwenye nchi zenye kipato cha juu
wananyonyeshwa maziwa ya mama kwa miezi 12.
o Kwenye nchi zenye
kipato cha chini na cha wastani, chini ya 40% ya watoto wachanga walio chini ya
miezi 6 wananyonyeshwa maziwa ya mama bila kuchanganyiwa chakula kingine, na
theluthi mbili za watoto kati ya miezi 6 na miaka 2 wanapata maziwa ya
mama.
Akina mama wana uwezekano wa
mara 2.5 zaidi kunyonyesha maziwa ya mama pale ambapo unyonyeshaji maziwa ya
mama unalindwa, unahamasishwa na unaungwa mkono.
·
Mipango ya kuunga mkono inajumuisha ushauri nasaha kwa mtu mmoja mmoja au elimu ya vikundi, kutoa msaada wa jinsi
ya kunyonyesha maziwa ya mama baada ya kujifungua, na mafunzo kuhusu maziwa ya mama
kwa ajili ya wafanyakazi wa afya.
·
Viwango vya kunyonyesha maziwa ya mama vinaweza kuboreshwa kwa kiasi
kikubwa kwa muda mfupi sana.Kifurushi chenyemiongozo ya kufundishia, sera na
mipango ya kusaidia akimama kwenye vituo vya afya, majumbani, na hata makazini vinaonyeshwa
kuwa na mchango mkubwa zaidi. Hivyo inatupasa:
o Kusambaza taarifa sahihikuhusu thamani ya kunyonyesha maziwa ya mama kama afua yenye nguvu kwa
ajili ya afya na maendeleo, yenye manufaa kwa watoto na akinamama.
o Kujenga mitazamo mizuri katika jamii kuhusu kunyonyesha maziwa ya mama na kusisitiza kuhusu kuwa na mtazamo chanya wa
kunyonyesha maziwa ya mama.
o Kuonyesha nia ya kisiasaya kuunga mkono unyonyeshaji maziwa ya mama.
o Kudhibiti tasnia ya chakula mbadala wa maziwa ya mama kwa kufuatilia na kutekeleza kisheria Kanuni ya
Kimataifa ya Uuzaji wa Chakula Mbadala ya Maziwa ya Mama.
oKueneza na kufuatilia mikakati
ya unyonyeshaji maziwa ya mama na mienendo katika kunyonyesha maziwa ya mama.
o
Kuimarisha hatua za kisera kuhakikisha sheria zinazowalinda wanawake katika kipindi cha uzazi zinaboreshwa
na afua za mahali pa kazi zinatekelezwa na kuwa huduma za afya na uzazi ni
rafiki kwa kuwawezesha kinamama kunyonyesha maziwa ya mama na zinafuata Kanuni.
Kujitoa na kuwekeza katika
afya wa wanawake na watoto – pamoja na kunyonyesha maziwa ya mama – kuwezesha
kufanikisha lengo la dunia litakalopelekea kuwepo na maendeleo katika malengo
mengine ya afya na maendeleo.
·
Kuwekeza kwenye kuinua ubora na utoaji huduma kwa maeneo mengi zaidi kwa
wanawake na watoto wao wachanga kutapelekea kupata faida ya mara tatu zaidi ya
mtaji, kwa kuzuia 54% ya vifo vya mama wajawazito, 71% ya vifo vya watoto
wachanga na 33% ya watoto wanaofia tumboni.
·
Afya ya wanawake, watoto na vijana ni mzunguko ambao husababisha mabadiliko
yanayohitajika ili kuunda hali ya afya ya baadaye yenye ustawi zaidi,imara
zaidi na endelevu kwa ajili ya kila mmoja.
·
Kumekuwa na maendeleo makubwa katika miaka 15 iliyopita hususani kwenye afya ya uzazi, mama mjamzito, watoto
wachanga, na vijana (RMNCAH), ambayo ni
muhimu katika kuendeleza Mkakati wa Dunia
wa Kuimarisha Afya ya Wanawake, Watoto na Vijana na malengo yake ya
Kuendelea Kuishi, Kustawi, na Kubadilika yakijumuisha harakati ya Kila Mwanamke Kila Mtoto. Kuendelea
kuishi, afya na ustawi wa wanawake, watoto na vijana ni muhimu katika
kutokomeza umaskini uliokithiri, kukuza maendeleo nauthabitina kutimiza Malengo mapya ya Maendeleo
Endelevu.
Mwaka huu The
Lancet imeandaa mkusanyiko wa ushahidi mpya ambao utakazia kwenye mada
muhimu zilizotajwa na Mkakati wa Dunia wa
Kuimarisha Afya ya Wanawake, Watoto na Vijana. Hii ni pamoja na kuzindua
Mfululizo wa makala kuhusu Watoto
Wanaofia Tumboni (imeshatolewa mwezi Januari 2016), Kunyonyesha Maziwa wa Mama (Januari 2016), ripoti kuhusu Tume ya
Afya na Ustawi wa Vijana iliyoandaliwa na The Lancet(itatolewa mwezi Mei,2016),
na baadaye kutakuwa na Mfululizo kuhusu
Afya ya Mama Mjamzito, Maendeleo na Makuzi ya Awali ya Mtoto, Afya ya Wanawake
na Mama na Mtoto Kuendelea Kuishi. Makala ya Kila Mwanamke Kila Mtoto itajulisha nchi na wabia kuhusu ushahidi
huu katika kusaidia utekelezaji wa Mkakati wa Dunia
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni