Alhamisi, 8 Januari 2015

Redds Miss Tanzania mshindi wa tatu Dorice Mollel atoa msaada wa vifaa vya kupumulia katika hospitali ya singida


Redds Miss central Zone 2014/15 Doris Mollel akisaini kitabu cha wageni katika hospitali ya mkoa Singida kabla ya halfla ya kukabidhi mashine mbili za kupumulia kwa watoto waliozaliwa kabla ya muda wa kawaida zenye thamani ya Tsh milioni 1.2. Waliopo nyuma ni warembo wengine wa Redds Miss Central Zone Linda Bureta, Blath Chambia na Suzy Wahere.

 Doris Mollel akisema Maneno machache wakati akikabidi mashine mbili za watoto kupumulia zenye thamani ya Tsh millioni 1.2 kwa hospitali ya mkoa wa Singida kwa ushirikiano na Manifester brand.

Doris akikabidhi mashine 2 za msaada wa watoto kupumulia zenye thamani ya Tsh milioni 1.2 kwa mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Singida Dk. Daniel Tarimo, msaada kwa ushirikiano na Manifester brand. Mgeni rasmi kwenye hafla hii alikua ni mkuu wa wilaya ya Singida Bi. Queen Mlozi (hayupo pichani).


Makabidhiano. Mashine mbili za msaada wa watoto kupumulia zilitolewa kwa ushirikiano na Manifester brand.


    Doris katika picha ya pamoja na mkuu wa wilaya ya Singida Bi. Queen Mlozi, Mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Singida Dk. Daniel Tarimo, Muandaaji wa Miss Singida Bi. Bora Lemmy na warembo wengine wa Redds miss Central Zone.


      Doris kwenye picha ya pamoja na warembo wenzake wa central zone walioenda kumuunga mkono. Linda Bureta, Blath Chambia na Suzy Wahere.
Akiwa na wafanyakazi wa wodi ya watoto

   Alipata nafasi ya kuwaona watoto hawa wawili wazuri kwenye wodi yao

   Kwenye picha nyingine ya pamoja

 Mtoto aliyezaliwa kabla ya muda wa kawaida akiwa kwenye mrija wa kumsadia kupumua uliounganishwa na mashine kama ambazo zimekabidhiwa na Doris.

   Alipata nafasi ya kuwasimulia baadhi ya kina mama waliojifungua watoto njiti kuhusu historia yake na kuwapa moyo kwamba hata watoto wao pia watakua na kufanikiwa kufika popote pamoja na kuzaliwa njiti.

  Wakiwa na nyuso za furaha.

Picha na Albert Manifester

Na mwandishi wetu, Singida


Katika kuianza safari yake ya huduma za jamii kwa mwaka 2015, Redds Miss central zone 2014-2015 Doris Mollel ametoa msaada wa mashine 2 za kupumulia kwenye hospitali ya mkoa wa Singida zenye thamani ya Tsh 1,200,000/=. Mashine hizo huwasaidia watoto waliozaliwa kabla ya muda wa kawaida (Pre-mature babies) katika mfumo wao wa upumuaji ambao huhitaji msaada wa juu zaidi mara tu wanapozaliwa.

Doris ambaye pia ni mshindi wa tatu wa Redds Miss Tanzania 2014 ni mwanaharakati wa dhana ya Urembo wenye Malengo endelevu kwa jamii ‘Beauty with a Purpose’. Amefanya kazi kubwa kwenye sekta ya elimu akijikita zaidi kwenye kuchangia Vitabu kwa shule za msingi na sasa, akiwa ni mmoja ya watu ambao walizaliwa kabla ya muda wa kawaida ameamua kupanua wigo wake wa huduma za jamii kuleta mwamko na kusaidia kuokoa maisha ya watoto hawa.

Akiongea kwenye hafla ya kukabidhi mashine hizo iliyofanyika hospitalini hapo, Mollel alisema. “Kiwango cha vifo kwa watoto wanaozaliwa kabla ya kukomaa ni karibu 30% vikichangiwa kwa kiasi kikubwa na ukosefu wa vifaa vya kutosha kusaidia mifumo yao ya upumuaji mara tu wanapozaliwa. Nikiwa moja ya watoto hao ambaye nilibahatika kupata msaada na huduma ya kutosha nilipozaliwa, Ninaelewa ni jinsi gani matunzo haya ya awali yalivyo muhimu kwenye kuokoa maisha ya watoto hawa na ninajikita kuwasaidia”

Bw. Albert Mbepera, Mkurungezi wa Albert Manifester Photojournalism; kitengo ndani ya Manifester brand kilichojikita kwenye masuala ya jamii alisema ‘huduma kwa jamii ni eneo muhimu sana kwetu. Tunafurahi kujitolea kufanya kazi na Doris katika maswala ya kusaidia jamii na tunaamini kuwa ushirikiano huu utasaidia kukusanya na kuonyesha matatizo ya wahitaji ili kuongeza uelewa na msukumo wa misaada kutoka kwa sekta binafsi na wanajamii kwa ujumla’

Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa ni mkuu wa wilaya ya Singida Bi Queen Mlozi na ilihudhuriwa na Mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Singida Bw. Daniel Tarimo, Daktari bingwa wa watoto wa Hospitali ya Singida, Muandaaji wa Redds Miss Singida 2014 Bora Lemmy na washindi wengine wa Redds Miss central Zone Linda Bureta, blath Chambia, Suzy Wahere.

Doris Mollel na Manifester brand wanapenda kuwashukuru ANUDHA PHARMACEUTICALS LTS kwa mchango wao mkubwa katika kufanikisha shughuli hii.
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Kumbukumbu la Blogu