Alhamisi, 8 Januari 2015

Mfuko wa Maendeleo ya Vijana wasaidia Vijana wa Mtwara kupata ajira

Kikosi kazimaalum kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo wa kiongea na Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara-Mikindani ,Bw. Rashid Mohamed walimpotembelea leo ofisini kwake kwa ajili ya kufuatilia na kufanya tathmini ya mikopo iliyokwishatolewa katika Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara-mikindani.
Wajumbe wa kikundi cha AMKENI kutoka Halmashauri ya manispaa ya Mtwara mikindani wakiwa katika majadiliano na wajumbe wa kikosi kazi maalum kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo walipowatembea leo ili kufanya ufuatiliaji na tathmini ya mikopo iliyokwishatolewa kwa kikundi hicho ilikujua nichangamoto gani wamekutana nazo ilikuboresha zaidi Mfuko wa Maendeleo ya Vijana.

Wajumbe wa Kikosi kazi kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo wa kiangalia magunia ya korosho ambayo kikundi cha AMKENI katika Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara kimeyapata kupitia mfuko wa Maendeleo ya Vijana ambao umewawezesha wanachama wa kikundi hicho kujiendeleza  kimaisha.

Mwenyekiti wa Halmshauri ya Mtwara Vijijini Bw. Musa Said akimkaribisha ofisini kwake kiongozi wa kikosi kazi kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Afisa uchumi mwandamizi Bw.Ngao Yohana walipotembelea wilaya iyo ilikufanya tathmini na ufuatiliaji wa mfuko wa Maendeleo ya Vijana.

Afisa Uchumi Mwandamizi kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo ,Bw.Yohana Ngao akiwa katika majadiliano na kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Mtwara Vijijini Bw.Oscar Ng’itu ilikujua maoni na changamoto wanazopata wana vikundi waliopata mkopo kupitia mfuko wamaendeleo yaVijana katika eneo lake.

Picha na Daud Manongi
 
Kikundi cha Vijana cha AMKENI kutoka katika Halmshauri ya  Manispaa ya Mtwara kimefanikiwa kujiajiri na kuutumia vyema mkopo waliopewa na Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo ili kuanzisha miradi mbalimbali waliyoomba kupitia mfuko wa Maendeleo ya Vijana.

Hayo yamesemwa leo na katibu wa kikundi cha AMKENI kilichopo chini ya saccos ya Halmashauri ya Mtwara Vijijini Bw.Iddi Saidi Dogoa alipokuwa akiwaeleza wajumbe wa Kikosi kazi kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo walipowatembelea ili kufanya ufuatiliaji na tathmini ya mfuko wa Maendeleo ya Vijana wilayani hapo.

Kikundi hicho kinajishughulisha na ubebaji wa mizigo na kilimo na walipewa shilingi milioni saba ili kufanikisha mradi huo.”tumefurahi sana kupata mkopo kutoka Serikalini,kwani umetuwezesha kujiajiri na hata kuajiri watu wengine na pia tumeweza kulipa kodi ili kuchangia maendeleo ya Taifa letu”Aliongeza Bw. Iddi.

Aidha kikundi cha AMKENI kimefanikiwa kutumia vyema pesa inayopatikana kama faida kujiendeleza zaidi kimaisha kwani wameweza kununua viwanja na sasaivi wanakikundi wana sehemu za kuishi binafsi,wanajiandaa pia kuanza kilimo cha mihogo kupitia faida waliyopata katika biashara zao za kila siku.

Naye Kaimu Mkurugenzi Halmshauri ya manispaa ya mtwara  Bw.Rashid Mohamed ameshauri serikali kuendelee kujenga utaratibu wa kusaidia vijana wasio na kazi rasmi ili kuepukana na bomu la ajira kwa Vijana,na pia mikopo hii iwe chini ya masharti ya benki ili kuiboresha zaidi ili marejesho yafanywe kwa wakati.

Aidha Katibu msaidizi wa kikundi cha vijana saccos(MTWAYODEN),BwMohamed Ngowe ameishukuru Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo kwa kuwatembelea na kujua matatizo na changamoto wanazopata ili kuwapatia suluhisho na kukazia kuwa Wizara iendelee kutoa mikopo hii kwa wakati ili Vijana zaidi wazidi kuona na wavutiwe kujiunga.

Mfuko wa maendeleo ya Vijana ulianzishwa Chini ya Sheria Na.21 ya mwaka 1961 kifungo cha 17(1) ukiwa na lengo la kuwasaidia Vijana kupata mikopo yenye masharti nafuu na kuwajengea uwezo kiuchumi ili waweze kuanzisha au kuimarisha miradi yaokwa lengo la kuwawezesha kujitegemea na kukuza uchumi wa nchi.






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Kumbukumbu la Blogu