Hayo
yamebainishwa na Mwakilishi wa Taasisi ya Sta Travel Abbass Karim wakati wa
monyesho ya Tanzania International Education Fair 2016 yanayoendelea jijini Dar
es Salaam.
Abbas
amesema kuwa taasisi yao imekuwa msaada mkubwa kwa Watanzania wanaopata fursa
ya kusoma nje ya nchi kwani wanatoa huduma ya usafiri ikiwa na punguzo maalum
la gharama za usafiri ili waweze kumudu gharama hizo.
Aliongeza
kuwa mpaka sasa Taasisi yake imetoa huduma ya hiyo kwa watanzania wengi nhasa
wanafunzi wanaoenda kusoma Kuala Lumpar Malyasia, London Uingereza, na
Guangzhou China.
Aidha
Abbas alisema kuwa pamojja na kutoa huduma hiyo kwa watanzania kumekuwa na
changamoto katika upatikanajji wa Viza kwa wateja wao na kupelekea kujitokeza
kwa usumbufu, hata hivyo Sta Travel imekuwa ikijitahidi kuwasaidia wateja wake
ili wakamilishe taratibu zao kwa wakati.
Kwa
upande wake mtanzania aliyenufaika na kupitia Taasisi hiyo Bw. Ally Abdallah
amesema kuwa binafsi anaipongeza taasisi hiyo kwa kuwa imemuwezesha kusafirikwa
gharama nafuu ambazo kwake zilikuwa rahisi kuzimudu tofauti na gharama halisi
ya usafiri kwa kawaida.
Sta
Travel ni Taasisi inayojihusisha na utoajji wa huduma ya kusafirisha wanafunzi
kwa gharama nafuu yenye punguzo maalum kwa leongo la kuwasaidia watanzania
kufikia ndoto zao bila kuwapo na kikwazo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni