Kampuni maarufu ya Simu Tecno
Mobile imefanya promosheni kubwa inayohusiana na simu yao mpya inayokuja nchini
hivi karibuni TECNO CAMON C9 katika eneo
la City Mall, Kisutu jijini Dar es Salaam.
Simu janja (smartphone) ya
TECNO CAMON C9 ndiyo simu yenye kamera bora zaidi inayokuja katika soko kwa
sasa hivyo katika promosheni hiyo Zawadi mbalimbali zimetolewa kwa washindi 100
ambao waliweza kuagiza simu hiyo mapema kuanzia 21 mwezi wa sita mpka 2 mwezi wa saba kwa kiasi cha shilingi elfu
thelathini (30,000) ambayo itamaliziwa simu ikifika kwa mtumiaji.
Akizungumza wakati wa
promosheni hiyo meneja wa mauzo wa TECNO Mobile Tanzania, Bw.Fred Kadinala
amesema kua TECNO inawajali watumiaji wa simu zake hivyo kuamua kuwapa zawadi
kubwa na kuwaruhusu waagize simu kwa bei ndogo ili wapate simu hiyo mapema
Zaidi.
Zawadi kubwa kama TV screen
yenye wa inchi 42 imetolewa kwa mshindi wa kwanza yenye thamani ya million moja
na nusu, washindi wengine akijishindia Carlcare VIP card yenye thamani ya
shilingi laki 3(300,000)
itakayomuwezesha kutengenezewa simu yake
bure mwaka mzima kwa tatizo lolote litakalotokea na pia kifurushi
maalumu cha zawadi kutoka kampuni ya Tecno.
Promosheni hiyo iliyoanza saa
nane mchana kwa michezo mbalimbali iliyowavutiwa watazamaji wengi baada ya hapo
washindi Zaidi ya mia moja waliojishindia zawadi mbalimbali ikiwemo
rice-cooker, jagi la umeme, oven, na vifurushi vya zawadi kemkem tokea kampuni
ya Tecno Mobile Tanzania.
Simu ya TECNO CAMON C9
inatajiwa kuingia sokoni rasmi kuanzia mwezi wa saba nchini Tanzania tayari kwa
mtu yoyote kuinunua na kufurahia uzuri wa kamera yake.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni