Jumapili, 1 Mei 2016

Wadau wa michezo waaombwa kuendelea kujitokeza na kuwekeza katika Riadha

Naibu Waziriwa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura akisalimiana na Rais wa Shirikisho la Mchezo wa Riadha Afrika Mashariki Mhandisi Sadick Ibrahim (katikati) jana jijini Dar es Salaam wakati wa ufungaji wa mashindano ya Riadha Afrika ya Mashariki kwa Vijana wenye umri chini ya miaka 20 jana jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Makamu wa Rais wa Chama cha Riadha Tanzania (RT) William Kallaghe.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura akiwapungia mkono washiriki wa mashindano ya Riadha Afrika ya Mashariki kwa Vijana wenye umri chini ya miaka 18 alipokuwa mgeni rasmi wakati wa ufungaji wa mashindano hayo jana jijini Dar es Salaam.Kulia ni Rais wa Shirikisho la Mchezo wa Riadha Afrika Mashariki Mhandisi Sadick Ibrahim na kushoto ni Makamu wa Rais wa Chama cha Riadha Tanzania (RT) William Kallaghe.

Naibu Waziriwa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura akisalimiana na Makamu wa Rais wa Chama cha Riadha Tanzania (RT) William Kallaghe jana jijini Dar es Salaam wakati wa ufungaji wa mashindano ya Riadha Afrika ya Mashariki kwa Vijana wenye umri chini ya miaka 18.Katikati ni Katibu wa Naibu Waziri Bibi. Anna Nkinda.
Makamu wa Raisi wa Chama cha Riadha Tanzania (RT) Bw. William Kallaghe akisoma taarifa fupi juu ya mashindano ya Riadha Afrika ya Mashariki kwa Vijana wenye umri chini ya miaka 18 mbele ya Naibu Waziriwa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura(kulia mwenye miwani) jana jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wa mashindano ya Riadha Afrika ya Mashariki kwa Vijana wenye umri chini ya miaka 18 kutoka nchi mbalimbali wakipita mbele ya Naibu Waziriwa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura(hayupo pichani) alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya ufungaji wa mashindano hayo jana jijini Dar es Salaam.
 
Washiriki wa mashindano ya Riadha Afrika ya Mashariki kwa Vijana wenye umri chini ya miaka 18 kutoka nchi mbalimbali wakiimba wimbo wa Taifa la Tanzania wakati wa  hafla ya ufungaji wa mashindano hayo jana jijini Dar es Salaam.


Naibu Waziriwa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura akimpongeza mmoja wa washiriki kutoka Tanzania ambao wamekuwa washindi wa kwanza kwa wanawake  mbio za relay mita mia nne mara nne alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya ufungaji wa mashindano ya Riadha Afrika ya Mashariki kwa Vijana wenye umri chini ya miaka 18 jana jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziriwa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura akimvalisha medali mmoja wa washiriki kutoka Kenya ambao wamekuwa washindi wa kwanza kwa wanaume mbio za relay mita mia nne mara nne  alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya ufungaji wa mashindano ya Riadha Afrika ya Mashariki kwa Vijana wenye umri chini ya miaka 20 jana jijini Dar es Salaam.
Mshindi wa kwanza wa mbio za mita 200 katika mashindano ya Afrika Mashariki kwa Vijana wenye umri chini ya miaka 20 Bw. Ally Khamis Ibrahim kutoka Zanzibar ( katikati) na akiwa katika jukwaa moja na washindi wa pili na watatu ambao wate wanatokea nchini Kenya.
Washiriki wa mashindano ya Riadha Afrika ya Mashariki kwa Vijana wenye umri chini ya miaka 20 kutoka Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mashindano hayo kufunga rasmi jana jijini Dar es Salaam.

Na mpiga Picha Wetu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Kumbukumbu la Blogu