Uwekezaji mkubwa zaidi kwenye kunyonyesha maziwa ya mama
kunaweza kusaidia maendeleo yakiuchumi na kuokoa maisha ya watoto wa Tanzania.
“Wanawake
wanakabiliana na vikwazo vingi katika kunyonyesha maziwa ya mama; sera na
mipango imara zaidi ya kitaifa ni muhimu katika kutokomeza vikwazo hivyo”
Dar es Salaam, Tanzania, Februari 29, 2016 – Mfululizompya wa makala zilizochapishwa na The Lancetunatoa ushahidi kuwa kuboresha unyonyeshaji wamaziwa ya
mama kunaweza kuokoa maisha ya zaidi ya watoto 820,000 kila mwaka duniani na
Dola za Kimarekani bilioni 300 kila mwaka.
“Katika kipindi cha miaka iliyopita kumekuwa na maendeleo katika kupunguza
vifo vya watoto na utapiamlo nchini Tanzania. Hata hivyo, watoto270 chini ya
miaka mitano wanakufa kila siku na karibu asilimia 40 ya watoto hao wanakufa
ndani ya mwezi mmoja wa kuishi. Kati ya watoto wanaonusurika, mtoto mmoja kati ya
watatu wanadumaa kwa sababu ya utapiamlo sugu. Watoto hawa wanakosa fursa zao katika
maisha. Hali duni ya lishe inaathiri uwezo wa mtoto kujifunza na pia uwezekano
wa mtoto huyo kutengeneza kipato akiwa mtu mzima. Lakini kuna afua zinazojulikana
zinazoweza kusababisha mabadiliko makubwa na kuhamasisha kunyonyesha maziwa ya
mama.” amesema Mwakilishi wa UNICEF nchini Tanzania, Bibi Maniza Zaman, wakati
akiongea na vyombo vya habari Dar es Salaam. “Mfululizo wa makala ya “The Lancet”unatoa ushahidi wenye
ushawishi kuhusu faida mbalimbali za kunyonyesha. Uwekezaji kwenye kulinda,
kukuza, na kusaidia unyonyeshajimaziwa ya mama kunaweza kuokoa maisha ya watoto
wa Tanzania, na hatimaye, kusaidia kukuza uchumi.”
Makala za“The Lancet”zinaonyesha kuwa kuna faida nyingi za kiafya za
kunyonyesha maziwa ya mama. Unyonyeshaji maziwa ya mama kwa kiasi kikubwa sana kunaweza
kuzuia karibu nusu ya matukio ya kuhara na theluthi moja ya maambukizo ya njia
ya hewa– zikiwa ni sababu mbili zinazoongoza kupelekea vifo kwa watoto walio
chini ya miaka mitano. Watoto wanaonyonyeshwa maziwa ya mama kwa kawaida
wanahitaji kupelekwa hospitali mara chache zaidi na kuwa na uwezekano mdogo wa kupata
maambukizo na magonjwa, pia wana uwezekano mdogo zaidi wa kuwa na uzito mkubwa
na kupata kisukari baadaye maishani mwao.
Kuna faida za kiafya kwa mama pia. Kwa
kila mwaka ambao mama ananyonyesha, uwezekano wa kupata saratani ya matiti ya hatua ya pili unapungua
kwa asilimia 6. Viwango vya sasa vya kunyonyesha maziwa ya mama tayari vinazuia
vifo karibu 20,000 vinavyotokana na saratani ya matiti kila mwaka duniani – idadi
hii inaweza kuwa kubwa zaidi kwa kuboresha mbinu za unyonyeshaji wa maziwa ya mama. Pia
kunyonyesha kwa muda mrefu zaidi kumehusishwa na kupungua kwa saratani ya mfuko
wa mayai.
Kuongeza viwango vya unyonyeshaji
maziwa ya mama katika jamii kuna faida za kiuchumi. Watoto wanaonyonyeshwa
maziwa ya mama wanapata matokeo mazuri zaidi kwenye vipimo vya upeo wa kiakili.
Kimataifa, imekadiriwa kuwa gharama zinazotokana na kuwepo na watoto wenye upeo mdogo zaidi wa kikakili unaohusishwa na
kutonyonyeshwa maziwa ya mama ni jumla ya takriban dola za kimarekani bilioni 300
kwa mwaka.Nchi zenye kipato cha chini na kipato cha wastani zinapoteza zaidi ya
dola za kimarekani bilioni70 kila mwaka.Nchi zenye kipato cha juu zinapoteza
zaidi ya dola za kimarekani bilioni 230 kila mwaka.
Hata hivyo, hapa Tanzania kuna
mikoa inayooyesha mwelekeo unaotia moyo.
Kwa mfano, mkoa wa Kilimanjaro, Tanga na Iringa ina asilimia 75 ya watoto
wananyonyeshwa maziwa ya mama ndani ya saa moja baada ya kuzaliwa.Zaidi ya nusu ya watoto wenye umri wa miezi 0-5
wananyonyeshwa maziwa ya mama pekee katika miezi 6 ya mwanzo wako katika mikoa
yaIringa, Kigoma, Morogoro, Singida, Katavi na Geita, huku
Kagera ikiwa na kiwango kikubwa zaidi cha asilimia 70.
Ili kuimarisha jitihada za kitaifa za kuboresha unyonyeshaji
maziwa ya mama, vikwazo vinavyowakabili wanawake wengi duniani kote pia
vinapaswa kushughulikiwa nchini Tanzania ikiwa ni pamoja na:
- Mapungufu kwenye uelewa wa watoa huduma ya afya ambayo yanawaacha wanawake bila taarifa au msaada sahihi;
·
Kukosekana kwa mifumo imara ya
msaada kwenye familia na jamii, pamoja na mila na tamaduni
zisizounga mkono kunyonyesha maziwa ya mama; na
- Likizo ya uzazi ya muda mfupi au kutokuwepo kabisa kwa likizo hiyo. Likizo ya uzazi ya muda mfupi inaweza kuongeza uwezekano wa kutonyonyesha maziwa ya mama au kuacha kunyonyesha maziwa ya mama mapema kwa asilimia 400;
Jambo lingine ni uuzaji usiofaa wa vyakula mbadala vya
maziwa ya mama (ikiwa na pamoja na maziwa ya kopo kwa ajili ya watoto wachanga)
na watengenezaji na wasambazaji ambao hutoa matangazo yanayohusiana na ulishaji
wa watoto wachanga hali inayodhoofishaunyonyeshaji
maziwa ya mama kama njia yenye ufanisi ya kuboresha afya katika siku za kwanza za maisha ya mtoto. Hapa
Tanzania, Kanuni yaUuzaji wa Chakula (Udhibiti wa Ubora) cha Mbadala wa maziwa
ya Mama na Bidhaa Teuleya mwaka 2013, inalinda unyonyeshaji. – ufuatiliaji na utekelezaji imara zaidi wa
Kanuni hiyo unahitajika. Wanawake wanaofanya kazi wanahitaji kusaidiwa kupitia
sheriazinazolinda uzazi zinazotosheleza. Kwa wanawake waliopo kwenye sekta
isiyo rasmi, kuna haja ya kuboresha mifumo ya misaada ya kifamilia na kijamii, na
kuandaa mazingira bora zaidi ya kufanyia kazi, ili kuokoa muda na nguvu za
wanawake waweze kufanikisha unyonyeshaji maziwa ya mama.
“Kunyonyesha maziwa ya mama ni njia ya asili zaidi, yenye ufanisi zaidi wa
gharama, iliyo rafiki zaidi kwa mazingira na rahisi zaidi tunayoijua ya kuwapa
watoto wote, tajiri au maskini, mwanzo mzuri zaidi kiafya wa maisha,”
alimalizia kusema Bibi Zaman. “Kuweka vipaumbele kwenye kuwekeza katika kukuza unyonyeshaji
maziwa ya mama ni pendekezo bora.”
###
Kuhusu
UNICEF
UNICEF hutetea haki na ustawi wa kila mtoto, katika kila
tunalolifanya. Kwa pamoja na wabia wetu, tunafanya kazi katika nchi na maeneo
190 kutafsiri ahadi hiyo katika hatua za utendaji, kujenga juhudi maalum katika
kuwafikia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi na waliotengwa kwa
manufaa ya watoto wote, kila mahali. Kwa taarifa zaidi kuhusu UNICEF na kazi
zake tembelea: www.unicef.org/tanzania
Kwa
taarifa zaidi, au kwa ajili ya mahojiano, tafadhali wasiliana na:
Sandra Bisin, UNICEF Tanzania, Simu ya Mkononi: +255 787 600079, sbisin@unicef.org
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni