Jumapili, 18 Januari 2015

Chama cha uzazi na malezi bora(UMATI) kupitia kituo chake cha vijana umati temeke watembelea kituo cha watoto yatima kurasini

Mkufunzi wa vijana kutoka kituo cha vijana umati temeke akiwafundisha vijana kuhusu hatua za ukuaji na athari zake.


Mwerimishaji rika kutoka kituo cha vijana umati temeke ambaye pia alikuwa mtoto yatima kituoni hapo akiwaeleza vijana umuhimu wa elimu


Afisa Vijana wa Kituo cha Vijana UMATI Temeke akikabidhi zawadi kwa mwakilishi wa watoto yatima wa kituo cha Kurasini jijin Dar es Salaam walipotembelea kituoni hapo jana

Afisa Vijana wa Kituo cha Vijana UMATI Temeke akikabidhi zawadi kwa mwakilishi wa watoto yatima wa kituo cha Kurasini jijin Dar es Salaam walipotembelea kituoni hapo jana



Wafanyakaz wa umati wakiwa na watoto yatima pamoja na walezi wa watoto yatima katika kituo cha watoto yatima Kurasini

 Chama cha uzazi na malezi bora(UMATI) kupitia kituo chake cha vijana umati temeke walitembelea kituo cha watoto yatima kurasini tarehe 17.1.2015 ili kutoa elimu ya afya ya uzazi na ujinsia kwa vijana hao ili kuwasaidia kuepuka vishawishi vya ngono na makundi rika ambayo si mazuri na yatakayoharibu mwenendo wao wa maisha ya baadae na afya zao kiujumla. Athari hizo ni kama mimba katika umri mdogo,kupata maambukizi ya ukimwi na magonjwa mengine ya ngono,kutumia vilevi na madawa ya kulevya n.k

Picha kwa Hisani ya Kituo cha Vijana,UMATI-TEMEKE

 

 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Kumbukumbu la Blogu