Jumamosi, 30 Aprili 2016

Vijana wahamasishwa kutumia Ujasiriamali Jamii hili kujiletea maendeleo

Mwenyekiti wa Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF) Bw. Erick Chrispin akizungumza wakati wa mkutano wa Jukwaa hilo unaofanyika kila mwisho wa mwezi jana jijini Dar es Salaam. Mada kuu katika mjadala huo ilikuwa ni “Jinsi gani Asasi zinawezakutumia Ujasiriamali wa Kijamii katika kuibua na kuhakikisha inafikia malengo yake”
Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi ya Open Mind Tanzania (OMT) ambaye pia ni Mratibu wa Programu ya Kukuza Ajira zenye staha jijini Dar es Salaam(YEID) Bw. Dominic Ndunguru akiwasilisha maada kuhusu misingi ya ujasiriamali wakati wa mjadala kuhusu  “Jinsi gani Asasi zinawezakutumia Ujasiriamali wa Kijamii katika kuibua na kuhakikisha inafikia malengo yake” jana jijini Dar es Salaam. Mjadala huo uliratibiwa na  Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF). 
Meneja Matukio na Ushirikiano wa Asasi ya Buni Innovation Hub Bi. Maryam Mgonja akielezea kuhusu namna asasi yao inavyofanya kazi wakati wa mjadala kuhusu “Jinsi gani Asasi zinawezakutumia Ujasiriamali wa Kijamii katika kuibua na kuhakikisha inafikia malengo yake” jana jijini Dar es Salaam. Mjadala huo uliratibiwa na  Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF). 
Afisa Mtendaji Mkuu wa Sema Tanzania Bw. Kiiya Joel Kiiya akifafanua jambo wakati wa mjadala kuhusu “Jinsi gani Asasi zinawezakutumia Ujasiriamali wa Kijamii katika kuibua na kuhakikisha inafikia malengo yake” jana jijini Dar es Salaam. Mjadala huo uliratibiwa na  Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF) 
Mmoja wa washiriki wa Mjadala kuhusu “Jinsi gani Asasi zinawezakutumia Ujasiriamali wa Kijamii katika kuibua na kuhakikisha inafikia malengo yake” ambayepia ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Bi. Liliani Kimaro akiwasilisha hoja walizozipata wakati wa majadiliana kwenye kundi lao jana jijini Dar es Salaam. Mjadala huo uliratibiwa na  Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF).
Mmoja wa washiriki wa Mjadala kuhusu “Jinsi gani Asasi zinawezakutumia Ujasiriamali wa Kijamii katika kuibua na kuhakikisha inafikia malengo yake akichangia mada wakati wa majadiliano jana jijini Dar es Salaam. Mjadala huo uliratibiwa na  Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF).
Baadhi ya washiriki wa Mjadala kuhusu “Jinsi gani Asasi zinawezakutumia Ujasiriamali wa Kijamii katika kuibua na kuhakikisha inafikia malengo yake” wakifuatilia mada wakati wa majadiliano jana jijini Dar es Salaam. Mjadala huo uliratibiwa na  Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF).
Mmoja wa washiriki wa Mjadala kuhusu “Jinsi gani Asasi zinawezakutumia Ujasiriamali wa Kijamii katika kuibua na kuhakikisha inafikia malengo yake”. Akifafanua namna ujasiriamali unavyo tegemea zaidi kuanza na wazo badala ya mtaji jana jijini Dar es Salaam. Mjadala huo uliratibiwa na  Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF).

Picha/Habari na: Frank Shija
Watanzania hasa vijana wameaswa kutumia mbinu za Ujasiriamali Jamii katika kukabiliana na changamoto za kimaendeleo miongoni mwa jamii zinazowazunguka.
Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (TASEF) Bw. Erick Chrispin wakati wa mjadala kuhusu Jinsi gani Asasi zinaweza kutumia Ujasiriamali wa Kijamii katika kuibua na kuhakikisha inafikia malengo yake” uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Chrispin amesema kuwa ilikutatua changamoto na matatizo ya kijamii vijana wanawajibu wa kufikiri namna ya kutumia changamaoto hizo kama njia mbadala ya kujipatia kipato kwani kufanya hivyo kunafaida kwa pande zote.
“Ujasiriamali Jamii ndiyo suluhu tena endelevu katika kukabiliana na changamoto za kimaendeleo katika jamii zetu,chukulia mfano kuna tatizo la maji, unachimba kisima unauza maji kwa gharama nafuu, jamii inapata maji hali kadharika na wewe unaingiza kipato.Huo ndiyo Ujasiriamali ninaoungelea.” Alisema Chrispin
Aidha aliongeza kuwa kwa kuona umuhimu wa Ujasiriamali Jamii Jukwaa hilo lilianzishwa ili kusahidia kutoa hamasa kwa vijana nchini waweze kushiriki na kubuni mambo mbalimbali katika kutekeleza dhana ya Ujasiriamali Jamii.
Alisema kuwa ni faraja kuwa jamii kwa kiasi kikubwa imeitikia katika kutumia aina hiyo ya ujasiriamali na hasa inatokana na msukumo wa soko huria na kupungua kwa wahisani katika kugharamia shuguli za kijamii.
Jukwaa la Ujasiriamali Jamii Tanzania (Tanzania Social Entrepreneurship Forum –TASEF)  lilianzishwa mwaka 2012 ikiwa ni kwa njia ya Mtandao na baada ya kupata wadau wengi mnamo mwaka 2015 TASEF ikazaliwa rasmi na mpaka sasa jumla ya mikutano 9 ya majadiliano katika mada mbalimbali imekwisha fanyika, mijadala hiyo ufanyika kila mwisho wa mwezi.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Kumbukumbu la Blogu