Alhamisi, 18 Februari 2016

Wekezeni katika sekta za michezo



Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akisalimiana na  Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye alipowasili katika Uwanja wa Ndani wa Michezo kabla ya kikao baina yake na wadau na viongozi wa vyama vya michezo  jana jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akielekeza jambo kuhusu mradi wa kuendeleza Uwanja wa Ndani wa michezo jana jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel na wa mwisho kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadick.

Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akimsikiliza kwa makini Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye alipowasili katika Uwanjwa wa Ndani wa Michezo kabla ya kikao baina yake na wadau na viongozi wa vyama vya michezo jana jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akifafanua jambo kabla ya kikao cha wadau wa michezo na Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa(hayupo pichani) jana jjijini Dar es Salaam.Kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bibi. Sophia Mjema, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadick, na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura.

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura akifuatilia maelezo kuhusu mradi wa kuendeleza eneo changamani la michezo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Bw. Makoye Nkenyenge jana jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akisalimiana na Rais wa Shirikisho la Mpira Miguu Tanzania (TFF) Bw. Jamal Malinzi walipokutana katika kikao baina ya viongozi hao na Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa (hayupo pichani) jana jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Bw.Dioniz Malinzi akizungumza wakati wa kikao cha viongozi wa vyama vya michezo na Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa (hayupo pichani) jana jijini Dar es Salaam.

Mmoja wa viongozi wa vyama vya michezo akichangia hoja wakati wa kikao baina yao na Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa (hayupo pichani) kilichofanyika katika ukumbi wa Uwanjja wa Taifa jana jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akakifurahia jambo baada ya kumaliza kikao na wadau na viongozi wa vyama vya michezo jana jijini Dar es Salaam.Kulia kwake ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel na wa mwisho kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Zawadi Msalla

Waziri Mkuu wa Jjamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) mara baada ya kumaliza kikao baina yake na vingozi wa vyama vya michezo jana jijini Dar es Salaam.Waliokaa kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Elisante Ole Gabriel, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye,Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa BMT Bw. Dioniz Malinzi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadick na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bibi. Sophia Mjema.

Waziri Mkuu wa Jjamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wadhamini wa michezo nchini mara baada ya kumaliza kikao baina yake na vingozi wa vyama vya michezo jana jijini Dar es Salaam.Waliokaa kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Elisante Ole Gabriel, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye,Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa BMT Bw. Dioniz Malinzi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadick na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bibi. Sophia Mjema.

Waziri Mkuu wa Jjamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa vyama vya michezo nchini mara baada ya kumaliza kikao baina yake na vingozi hao jana jijini Dar es Salaam.Waliokaa kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Elisante Ole Gabriel, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye,Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa BMT Bw. Dioniz Malinzi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadick na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bibi. Sophia Mjema.


Picha zote na Frank Shija
Na Lilian Lundo


Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa ameyataka makampuni na wafanyabiashara kutangaza biashara zao kupitia uwanja wa Taifa.

Mhe. Majaliwa aliyasema hayo katika mkutano wa wadau wa michezo wakiwemo wadhamini wa michezo, vyama vya michezo vya Taifa na mashirikisho  uliofanyika katika moja ya kumbi zilizopo uwanja wa Taifa.
“Uwanja wetu una hadhi ya kimataifa lakini uwanja huu hautumiki kutangaza biashara yoyote  kama chanzo cha mapato, badala yake kuta za  uwanja  zimezungukwa na giza hasa muda cha usiku,” alisema Mhe. Majaliwa.
Mhe. Majaliwa aliongeza kwa kusema kuwa  kama uwanja huo utazungukwa na mabango ya matangazo yataupandisha  hadhi  na kubadilisha mandhari ya uwanja hasa muda wa usiku na  fedha zitakazopatikana zitatumika kuboresha uwanja huo.
Hivyo Mhe. Majaliwa amewataka wadhamini wa michezo kujitokeza kwa wingi kutumia fursa hiyo ya kutangaza bidhaa au huduma wanazozitoa kupitia uwanja wa Taifa ambao hutumika katika mechi nyingi za kitaifa na kimataifa zinazochezwa nchini.
Aidha, Mhe. Majaliwa amesema kuwa Tanzania itaendelea kupata heshima kupitia sekta ya michezo kwani michezo ni kielelezo kinachoweza kutambulisha utamaduni wa Taifa hivyo wadau wa michezo washikamane na Serikali na kuona ni namna gani matatizo ya michezo yatatatuliwa na michezo kuendelezwa nchini.
Serikali ya awamu ya tano imejipanga kuendeleza michezo nchini kwa kuweka misingi imara ya kuendeleza michezo kuanzia umri wa chini, kurekebisha sera na sheria za michezo ziliopitwa na wakati, kujali mafanikio, matatizo na mambo muhimu yanayohusu michezo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Kumbukumbu la Blogu