Jumatano, 1 Oktoba 2014

CHUO CHA SERIKALI ZA MITAA – HOMBOLO CHAPIGA HATUA KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZAKE. HAYO YAMEBAINIKA KATIKA KIKAO CHA BODI YA WADHAMINI YA CHUO CHA SERIKALI ZA MITAA HOMBOLO KILICHOFANYIKA TAREHE 25-26 AGOSTI 2014 KATIKA UKUMBI WA MIKUTANO YA BODI


Baadhi ya wajumbe na Sekretarieti kama wanavyoonekana katika picha

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Chuo cha Serikali za Mitaa Bw. Ramadhani H Khalfan akisisitiza jambo, kulia kwake ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi Mhe. Mgana Msindai na kushoto ni katibu wa Bodi ambaye ni Kaimu Mkuu wa Chuo Bw. Muriri Joseph

Majengo matatu awamu ya kwanza ya kituo cha afya yaliyokamilika kwa 95% kama yanavyoonekana katika picha 

Picha na Sebera Fulugence



Bodi ya Wadhamini ya Chuo Cha Serikali za Mitaa chini ya Mwenyekiti wake Bw. Ramadhan H Khalfan ilifanya kikao chake cha saba tarehe 26.08.2014 Chuoni Hombolo. Pamoja na kutanguliwa na vikao vya kamati ya Taaluma ya Bodi na Kamati ya Mipango, Fedha na Utawala vilivyofanyika tarehe 25.08.2014

Taarifa mbali mbali za utekelezaji wa Shughuli za Chuo kwa muda wa Mwaka  Julai 2013 – Juni 2014 ziliwasilishwa kwa Bodi ya Wadhamini.
Baadhi ya mafunzo yaliyofanywa na Chuo kupitia Idara ya Utafiti, Ushauri na Mafunzo ya Muda Mfupi kwa kipindi cha mwaka 2013/2014 ni yafuatayo:-
a)      Mafunzo ya kuwajengea uwezo Watunza kumbukumbu, Wahudumu, Wasimamizi wa Ofisi na Makatibu Mhutasi wa halmashauri na taasisi zingine za Serikali yalifanyika hapa Chuoni.
b)      Mafunzo kuhusu Sheria Mpya ya Manunuzi ya mwaka 2011 na kanuni zake za mwaka 2013, kwa Wakuu wa Idara na waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto.
c)      Mafunzo ya Uongozi na Utawala Bora kwa Wakuu wa Idara na waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.
d)     Mafunzo ya stadi za Menejimenti na Uongozi kwa Halmashauri za Wilaya za Kibondo na Kasulu.
e)      Tathmini ya Mahitaji ya Mafunzo kwa watumishi wa Halmashauri za Wilaya za Mkuranga, Kigoma, Kasulu, Kibondo na Manispaa ya Kigoma, Kazi ya Ushauri (Consultancy) chini ya Shirika la Maendeleo la Ubelgiji (BTC)
f)       Mafunzo ya Utunzaji kumbukumbu na Usimamizi wa Ofisi kwa Watumishi wa Wilaya ya Rombo.
g)      Mafunzo ya Uwajibikaji wa Kijamii (Social Accountability) kwa Watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, Asasi za Kiraia na Mashirika ya dini kutoka Wilaya za Karagwe, Ukerewe na Magu.
h)     Kuhusu uanzishaji wa Kozi za Shahada (Bachelor Degree), Bodi ya Wadhamini kupitia kamati yake ya Taaluma iliiagiza Menejimenti kuandaa andiko la hoja ya msingi kuhusu pendekezo hili na uwezekano wa kutoa mafunzo ya kujenga weledi na stadi za kazi kwa Watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kupitia kozi za Shahada.
Aidha, miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa ni pamoja na taarifa ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Chuo cha Serikali za Mitaa kwa mwaka wa masomo 2014/2015. katika mwaka wa masomo 2014/2015 jumla ya wanafunzi wapya 1803 wamechaguliwa kujiunga na kozi mbalimbali zitolewazo na Chuo cha Serikali za Mitaa. Idadi hii inajumuisha wanafunzi waliochaguliwa moja kwa moja na wale waliochaguliwa kupitia kozi ya “Pre-entry).
JEDWALI LIFUATALO LINAONESHA IDADI YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA
Na.
KOZI
ME
KE
JUMLA
1.       
Astashahada ya Utawala katika Serikali za Mitaa (BTCLA)
165
170
335
2.       
Astashahada  ya Uhasibu na Fedha katika Serikali za Mitaa (CLF)
36
19
55
3.       
Astashahada ya Maendeleo ya Jamii (BTCCD)
69
152
221
4.       
Astashahada ya Menejimenti ya Rasilimali Watu (BTCHRM)
46
78
124
5.       
Stashahada ya Utawala katika Serikali za Mitaa (DLA)
76
124
200
6.       
Stashahada  ya Uhasibu na Fedha katika Serikali za Mitaa (DLF)
45
43
88
7.       
Stashahada ya Maendeleo ya Jamii (DCD)
79
150
229
8.       
Stashahada ya Menejimenti ya Rasilimali Watu (DHRM)
44
61
105
9.       
Wanafunzi wa “Pre-entry course”
152
294
446

JUMLA
712
1091
1803

Katika mwaka wa fedha 2013/2014, Chuo kilipanga na kutekeleza miradi ya maendeleo kama ifuatavyo:-
1)      Ulipaji wa Fidia wa Eneo jipya (ekari 637)
Hadi mwisho wa Robo ya Nne ya mwaka wa fedha 2013/2014, Chuo kilikuwa kimepokea jumla ya Sh.200,000,000 kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi ambao walikuwa katika mpango wa kulipwa.  Vile vile, Chuo kilipokea Sh.350,000,000 kupitia ruzuku ya matumizi mengineyo kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi waliokuwa wamebaki kulipwa fidia katika bajeti ya mwaka wa fedha 2012/2013. Kwa mantiki hiyo, Chuo sasa kimelipa fidia ya eneo lote jipya lenye ukubwa wa ekari 637.
2)      Ujenzi wa Kituo cha Afya (Awamu ya Kwanza)
Ujenzi wa kituo cha Afya ( Awamu ya kwanza) ambao ulianza tarehe 09/09/2013 kwa kuhusisha majengo matatu ambayo ni Maabara (Laboratory Block), Matibabu (Treatment Block) na Watabibu (Consultation Block) umekamilika kwa 95%
Chuo cha Serikali za Mitaa ni miongoni mwa Taasisi zilizoko chini ya OWM-TAMISEMI na kilianzishwa kwa mujibu wa Sheria Na. 26 ya mwaka 1994 (Sura ya 396 toleo lililorejewa mwaka 2002). Lengo kuu la kuanzishwa kwake ni kuziwezesha Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini kutoa huduma bora zitakazowajengea wananchi uwezo wa kuimarisha utawala bora, kuondokana na umaskini na kuboresha maisha yao. Pia Chuo ni Taasisi Kiongozi ya Mafunzo (Lead Training Institution) kikiwa na majuku ya kuratibu mafuinzo yote yanayotolewa kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa, Kudhibiti ubora wa Mafunzo yanayotolewa kwa Mamlaka za Serikali za Mitaala na kuandaa Mitaala mbali mbali yakufundishia.
Majukumu ya Chuo yamegawanyika katika sehemu kuu tatu:-
Kutoa mafunzo ya muda mfupi na mrefu juu ya taaluma, ujuzi, stadi na mbinu za uendeshaji wa Serikali za Mitaa kwa Viongozi na Watumishi walio katika ngazi mbalimbali za Serikali za Mitaa;
Kutoa mafunzo juu ya mabadiliko yanayohusu Serikali za Mitaa kulingana na Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa na;
Kufanya utafiti na kutoa ushauri kwa Serikali Kuu, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Mashirika na watu binafsi juu ya masuala yote yanayohusu Serikali za Mitaa.



BODI YA WADHAMINI ILIPISHA WATUMISHI WANAOENDA MASOMONI
MWAKA WA FEDHA 2014/2014 KAMA IFUATAVYO
S/N
JINA
KOZI ANAYOENDA KUSOMA
UFADHILI
IDARA ANAYOTOKA

1.

Natangalia Kalimangasi


PhD

Chuo

Taaluma

2.

Jonas Kapwani


Masters

Chuo

Taaluma

3.

Isdory Nyoni


Masters

Chuo

Taaluma

4.

Cyprian Mbugano


Masters

Chuo

Utawala

5.

Grace Majura


Diploma

Chuo

Utawala

6.

Veronica Nahodha


Bachelor

Chuo

Utawala

 
                              Imetolewa na:                                
Public Relations Officer
Chuo Cha Serikali za Mitaa, Hombolo Dodoma
12.09.2014

 




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Kumbukumbu la Blogu